music

HANS%20MBEDULE%20BLOG

Thursday, February 7, 2013

WANAUME WATAKIWA KUACHA TAMAA ZA FISI. NANI KASEMA BOFYA HAPA

WANAUME wamekumbushwa kujenga tabia ya kuwa na aibu na kuacha tamaa ya kuoa wanawake ambao hawajafikisha umri wa miaka 18.
Wito huo ulitolewa jana bungeni na Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto Ummi Mwalimu wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu, Dk Mary Mwanjelwa (CCM) ambaye alihoji kama Serikali haioni kuwa ni wakati mwafaka kubadilisha Sheria ya Ndoa ili umri wa kuolewa utoke miaka 14 na kuwa 18.
Katika swali hilo Mwanjelwa aliitupia lawama Serikali kuwa imekuwa ikichangia kwa sehemu kubwa vifo vya wanawake ambao vingi vinatokana na kuzaa katika umri mdogo.
Naibu Waziri alisema kifungu cha 13 (1) cha Sheria ya Ndoa sura ya 29, kinasema kuwa mwanamume mwenye umri wa chini ya miaka 18 na mwanamke mwenye umri wa chini ya miaka 15 hawaruhusiwi kufunga ndoa na mtu yeyote lakini akasema kifungu cha 13 (2) kinaipa Mahakama mamlaka ya kufungisha ndoa baada ya maombi maalumu.
Alisema Mahakama inaweza kutoa kibali hicho endapo waombaji wamefikisha umri wa miaka 14 na Mahakama ikiridhika kwamba yapo mazingira maalumu yanayohitajika wenye umri huo kufunga ndoa.
“Vilevile kifungu cha 17 (1) kinampa fursa mtoto wa kike mwenye umri wa chini ya miaka 18, kupata ridhaa ya kuolewa kutoka kwa mzazi wake au mlezi wake endapo baba au mama watakuwa wamefariki,” alisema Mwalimu.
Hata hivyo alikiri kuwa Serikali inatambua kuwa watoto wengi wamekuwa wakiolewa chini ya umri uliowekwa na sheria na mara zote hatua za kisheria zimekuwa zikichukuliwa dhidi ya wazazi, walezi na wanaume wanaowaoa wasichana hao.     

No comments:

Post a Comment